19 Julai 2026 - 02:34
Kiongozi wa Iran: Ukiukaji wa Marekani unathibitisha saini yake haina thamani; Iran ina masomo yasiyosahaulika kwa adui

Katika ujumbe kuhusu kuaga kwa kishujaa kwa Kiongozi shahidi wa Iran, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Mojtaba Khameni amesema kuwa ukiukaji wa mara kwa mara wa Marekani wa makubaliano yaliyosainiwa kati ya marais wa Iran na Marekani umeonyesha tena kuwa saini ya rais wa Marekani haina thamani. Amesema pia kuwa Iran na mhimili wa muqawama wana masomo yasiyosahaulika kwa adui, kama ilivyoonekana kupitia ujasiri wa wapiganaji na uhodari wa wananchi wa maeneo ya kusini.

Shirika la Habari la la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Katika ujumbe kuhusu kuaga kwa kishujaa kwa Kiongozi shahidi wa Iran, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Mojtaba Khameni amesema kuwa ukiukaji wa mara kwa mara wa Marekani wa makubaliano yaliyosainiwa kati ya marais wa Iran na Marekani umeonyesha tena kuwa saini ya rais wa Marekani haina thamani. Amesema pia kuwa Iran na mhimili wa muqawama wana masomo yasiyosahaulika kwa adui, kama ilivyoonekana kupitia ujasiri wa wapiganaji na uhodari wa wananchi wa maeneo ya kusini.

Katika ujumbe wake, Ayatollah Sayyid Mojtaba Khameni alisema kuwa ukiukaji wa Marekani wa Makubaliano ya Maelewano ya Islamabad unaonyesha wazi kwamba uonevu, ubabe na ukatili ni sehemu zisizotenganishwa na itikadi ya Marekani. Alisema hatua hizo zimefichua tena sura halisi ya Washington na kutoa ushahidi mwingine wa udanganyifu, kutokuaminika na uovu wa Marekani.

Aidha, alionya kuwa Marekani inapojaribu kuongeza mivutano na kudhalilisha zaidi Iran, inapaswa kujua kwamba taifa la Iran na mhimili wa muqawama wana masomo yasiyosahaulika kwa adui. Alisisitiza kuwa ujasiri wa wapiganaji na uthabiti wa wananchi wa maeneo ya kusini ni ushahidi wa wazi wa uwezo huo.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha